Skip to main content

THAMANI YA POGBA NI EURO SIFURI




ETI  POGBA  ANADAI  THAMANI  YAKE IMESHUKA.
TURIN, ITALIA




KIUNGO  Paul  Pogba  ametoa  kali baada  ya  kudai  kwamba  anadhani  thamani  yake  kwa  sasa  ni Euro  sifuri  kwa  sababu  bado  hajafanya  chochote  cha  maana   kwenye  mchezo  wa  soka.
Staa  huyo  wa  Ufaransa  juzi  Jumapili  alionyesha  kiwango  cha  hali  ya  juu  wakati  Juventus  ilipoichapa  Hellas  Verona  mabao  4-0, ambapo  naye  alifunga.
Wakala  wake  mapema  wiki  hii  alisema  kwamba  mchezaji  huyo  anapaswa  kuhama  hivi  karibuni  kwa  sababu  ndicho  kipindi ambacho  yupo  kwenye  ubora  wake  jambo  ambalo  Pogba  mwenyewe  halioni  kama  ni  kweli  kwa  sababu  hana  alichokifanya  kwenye  soka.
Staa  huyo  wa  zamani  wa  Manchester  United  alisema  thamani  yake  ipo  chini  hadi  atakapo  pandisha  kiwango cha  soka  lake  na  kufanya  mambo  ya  maana.
“ Thamani  yangu  ni  Pauni  0.Sina thamani  labda  kama  ntabadili  kiwango  change  cha  kucheza  soka  la  hali  ya  juu “ alisema  na  kuongeza.
“Ndoto zangu  ni  kutwaa  tuzo  ya  Ballon d’Or  hapo  baadaye, lakini  hilo  ni  lazima  nilifanyie  kazi  sana. Nataka  kuwa  kama  Andrea  Pirlo.

CREDIT : GAZETI  LA  MWANASPOTI

Comments