Skip to main content

BAADA YA ONYO LA P-SQUARE,DAVIDO KUTUMIA MILIONI 450 KUMMALIZA DIAMOND!!! KUFANYA NYIMBO YA KIHISTORIA NA ALI KIBA


Davido  na  Diamond
SASA  ni  nguvu  ya  pesa! Kuna  usemi  wa  kiswahili  unaosema  kuwa  vita  vya  panzi  ni  furaha  kwa  kunguru.   Ukweli wa  usemi   huu  umejidhihirisha  hivi  karibuni  baada  ya  gazeti  hili  kunasa  habari  kuwa  mkali  kutoka  nchini  Nigeria, Davido  amepanga  kutumia  kiasi  cha  milioni  450  kwa  ajili  ya  kufanya   nyimbo  ya  pamoja  na  Ali  Kiba  akiwa  na  lengo la  kuvunja  kabisa  ufalme  wa  Diamond.



Ali  Kiba.

Habari  hii  imekuja  muda  mfupi  tangu  kundi  mahiri  Afrika  linalo  undwa  na  mapacha  kutoka  nchini  Nigeria  Peter  na  Paul  au  "P-Square" kutangaza  kuwa  kama  Davido  anataka  kuendelea  kutamba  kwenye  ramani  ya  muziki  basi  ni  bora  akajiweka  pembeni  na  Diamond.

Kauli  hii  ya  P Square  inaonekana  kumkera  sana  Davido  na  sasa  moja  katika  mipango  yake  ni  kutumia  kiasi  kinacho  kadiriwa  kufikia  milioni  450  za  kitanzania  kufanya  nyimbo  ya  pamoja  na  mkali  mwingine  kutoka  Tanzania   Ali  Kiba.

Davido  ana  amini  anaweza  kutumia  bifu  la  chini  kwa  chini  baina  ya  Ali  Kiba  na  Diamond  kurudisha  heshima  yake  inayo  anza  kupotea  tangu  ajiingize  kwenye  malumbano  na  Diamond.

Ikumbukwe  kuwa  Davido  na   Diamond  walikuwa  marafiki  wakubwa  kiasi  cha  Diamond  kuamua  kufanya  nae  remix  ya  wimbo  " My  Number  One "  ulio fanya  vizuri  barani  Afrika  na  kuweza  kutwaa   tuzo  ya  wimbo  bora  wa  kushirikisha  Afrika.
CHANZO : GAZETI  LA LETE MAMBO.

Comments