Skip to main content

MADHARA YA KUBANA MKOJO KWA MUDA MREFU



Watu wengi huvumilia mkojo kwa muda mrefu kutokana na sababu mbalimbali. Baadhi wanaweza wakawa katika eneo ambalo hawezi kwenda haja ndogo lakini wengine ni uzembe ambapo wengi utakuta anaangalia tamthilia hivyo hataki apitwe, au anaona akienda haja ndogo hadi arudi umbea unaopigwa utampita na hivyo anaamua kubana mkojo, hayo yote yana madhara kwa mwili wako.


Je! Wewe hukojoa mara ngapi kwa siku? Mbili?, Tatu? Tano? Kwa mujibu wa watalaamu mbalimbali, wamesema kuwa kila mtu anatakiwa kukojoa kila baada ya saa 4 hadi 6, lakini kama utashikilia mkojo wako kwa muda zaidi, utakuwa uanajiweka kwenye hatari ya kukumbwa na matatizo mbalimbali.


Haya ni baadhi ya madhara yatakayokupata endapo utabana mkojo kwa muda mrefu zaidi;


1. Kujikojolea


Kwa mujibu wa Daktari Lauren Streicher akifafanunua hili alisema kwamba, mtu anapaswa kufikiria kibofu chake kama puto ambalo limejazwa maji kupitiliza. Puto hilo likatanuka hadi mwisho wake na kuwa zito, kadiri utakavyokuwa unazidi kuubana, ndivyo itakavyokuwa vigumu kwako wewe kutembea hadi chooni kabla hujajikojolea.


Itakuwa ni aibu kwa mwanamke mtu mzima kujikojolea eti kwa sababu hakwenda chooni kwa kunogewa na muvi au umbea ambapo pengine hauna faida.


2. Kulegea kwa misuli ya Pelvic





Misuli ya Pelvic hutumika katika kuzuia mkojo usitokea au kuuruhusu utoke katika kibofu cha mkono. Ukiwa na tabia ya kubana mkono kwa muda mrefu sana, misuli hii itachoka na hivyo kuacha kufanyakazi kwa usahihi. Hilo linapotokea unashindwa kuzuia tena mkojo wako sababu misuli imelegea na hivyo mkojo ukija unapita moja kwa moja.


Hivyo, epuka kuharibu misuli hiyo kwa kubana mkojo kwa vitu ambavyo sio vya msingi. Kila unapohisi mkojo nenda kakojoe kisha rudi, endelea na ulichokuwa unafanya.


3. Maumivu


Kwa kawaida unaposhikilia mkojo kwenye kibofu kwa muda mrefu, unapatwa na maumivu makali, lakini maumivu hayo hutokomea mara tu unapokwenda haja ndogo. Maumivu hayo yanaweza yakawa ni mfumo wako wa maisha kama hutachukua tahadhari mapema.


Waswahili husema kuwa, tabia hujenga mazoea, na hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa misuli ya mwili wako, ukizoea kubana mkojo kila mara, itakua ikiima kila mara.


4. Kutanuka kibofu


Basi tusema kwamba ukibana mkojo kwa muda mrefu, kibofu chako kinaweza kisipasuke kutokana na wingi wa mkojo lakini kikatanuka kuliko ukubwa wake unaotakiwa.


Tatizo la kutanuka kwa kibofu kutokana na kubana mkojo mara kwa mara ni kwamba mwili wako utakuwa haukupi taarifa kuwa unatakiwa kwenda kujisaidia. Hii ni kwa sababu umbo la kibofu limeongezeka. Taarifa hizo ambazo hutolewa na ubongo wakati kibofu kimejaa ni muhimu sana, lakini kibofu kikitanuka hutozipata.


Ni kweli wakati mwingine unaweza ukabanwa na mkojo na kuwa sehemu ambayo huweza kupata msaada ya kujisaidia, lakini epuka tabia hii kuwa mazoea.

Chanzo: Swahili Times  &  JF

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA