Skip to main content

MREMBO AWA ONYA WANAWAKE WANAO WAHUDUMIA NA KUWAHONGA WANAUME. SABABU YAKE ITAKUSHANGAZA.


Image result for IMAGES  SHOWING  AN AFRICAN COUPLE


 MWANAUME KUMHUDUMIA MWANAMKE NI SEHEMU YA NGUVU ZA KIUME, DADA YANGU ACHA KUWA MWANAUME!
Mrembo  mmoja, kupitia  ukurasa  wake  wa  facebook, ameweka  ujumbe  unao  wataka  wanawake  wenye  tabia  ya  kuwahonga  na  kuwahudumia  wanaume  zao, kuacha  mara  moja  tabia hiyo kwa madai  ya  kwamba, kuhonga  na  kumuhudumia  mwenza   ni  jambo  linalopaswa  kufanywa  na  mwanaume  na  sio  mwanamke.

Maelezo  ya  mwanadada  huyo, yanasomeka  kama  ifuatavyo :

Hii ni Dada zangu ambao mmegeuka wanaume katika mahusiano yenu, mnapaswa kujua kuwa hakuna mwanaume ambaye napenda kuoa mwanamke ambaye anamhudumia.

Hapa mnielewe sio mwanmke ambaye anamzidi kipato hapana, unaweza kumzidi kipato mume wako lakini usimhudumie, kwamba kuna wale wanaume ambao;

Anaendesha gari la mkewe, anaomba hela ya chakula kwa mke, wazazi wakiumwa ni mke, ada ni kutoka kw, akitaka kutoka out ni mke yaani hata kama anafanya kazi lakini hachangii kitu katika familia. Na kama ni mpenzi wako tu hata si mume basi wewe hajawahi kukupa hata hela ya Pedi lakini kila akiwa na shida ni kukulilia.

Tena kama mwanamke ambaye anaomba hela ya saluni ambaye ukimnyima ananuna, yaani una boyfriend anakuomba hela ukimnyima ananuna.
 Dada yangu jua huyo hatakuja kukuoa, narudi hatakuja kukuoa na kama ikatokea bahati mbaya akakuoa narudia kama itatoke bahati mbaya naruidia tena kama itatoke bahati mbaya atakuoa basi jua kuwa utakua na msaidizi tu.

Kwamba mwanaume kumhudumia mkewe au mpenzi wake ni sehemu ya nguvu za kiume, kwamba huwezi kujiita mwanaume mbele za watu kama kila kitu unamtegemea mkeo, maamuzi yote ni mke. Sasa ili uwe na kauanaume hata kambali ni lazima uwe na kamchepuko flani ambako unakahonga, ambako kanakuambia Pedi zimeisha, kana shida ya hela ya saluni na ambako kanaweza kununa ukikanyima hela.

Ndiyo ilivyo hili ni suala la kisaikolojia upende usipende hivyo Dada yangu hembu acha upumbavu, narudia acha upuuzi wa kuhonga honga wanaume.

Hapa mnielewe kusaidiana na mpenzi wako ni raha na ni kitu kizuri sana, kwamba kama ukiwa na shida anakusaidia bila kusitasita basi hata yeye akiwa na shida msaidie.

Kama yeye anakununulia kitu na kukupa zawadi bila hata kuombwa na wewe fanya hivyo hayo ndiyo mapenzi.

Lakini Dada yangu kama ukimuomba vocha ya buku atakuambia matatizo mpaka ya marehemu Bibi yake, hakupi au unaomba vocha leo halafu anakupa baada ya mwezi huyo hata akilazwa Hospitalini usimnunulie panado.

 Kwanza ni mwanaume gani huna hata hela ya vocha halafu unatafuta wanawake, kwani sabuni ziko wapi, nenda kanunue JAMAA kama watoto wenzako.


Sasa mimi nishachoka kuandika, sasa wewe jifanye unapendwa unachukua mpaka na mkopo eti kuhudumia mwanaume mtu mzima na midevu yake, eti anakudnaganya anasoma yuko chuo umlipie! Pumbavu yaani umlipie mwanaume ada, unaakili Dada yangu! Kwani Baba yake yuko wapi, aende akafanye kibarua kama wanaume wenzake ajisomeshe. Sasa wewe lipa ila ukishadhulumiwa ukachwa unakaribishwa kusoma na Kitabu changu!
Top of Form



             MAKALA NYINGINEZO

JINSI  KISUKARI  KINAVYO  SABABISHA  MARADHI  YA  NGUVU  ZA  KIUME


JINSI  KITAMBI  KINAVYO PATIKANA  NA  JINSI  UNAVYO WEZA  KUKIONDOA  KWA  TIBA  ASILIA


JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU  NA  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME

IJUE  SAYANSI  YA  NGUVU  ZA   KIUME

UHUSIANO  KATI  YA  UNENE  ULIO  ZIDI  NA  TATIZO  LA  UKOSEFU  NA  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZAP  KIUME


KISA  UGONJWA  WA  KISUKARI  MWANAMKE  AMKIMBIA  MUMEWE  WA  NDOA  NA  KWENDA  KUISHI  NA  JIRANI


KUTANA  NA  MWANAMKE    AIYE  JITOLEA  KUMTIBU   MUMEWE  MARADHI  YA  AJABU


PUNYETO  ILISABABISHA  NINUSURIKE  KWENDA  JELA


Comments